top of page

Unabii 24“Watoto, Kuweni Kamili Kama BABA Wenu Duniani, ili Kustahimili Tanuru ya BWANA!

Umepewa Nabii Hannah kwa Sifa, Heshima & Utukufu wa ELOHIM (MUNGU) Mbinguni


Umeandikwa 24 Februari, 2019


Muhtasari

Hukumu itakayokuja kama Siku 3 za Giza itakuja tena na katika ufunuo 6:12 “Kisha nikatazama na wakati MWANAKONDOO Alipovunja Mhuri wa sita, kukawa na tetemeko kubwa la ardhi; jua likawa jeusi kama gunia la manyoya; mwezi wote ukawa mwekundu kama damu.” Hili ni tukio lenye maafa linalokuja, lilia BWANA YAHUSHUA leo kwa ajili ya Wokovu, kesho inaweza kuwa ushachelewa zaidi!


Ujumbe wa Kinabii


(Nilisikia BWANA Akizungumza katika maombi yangu ya asubuhi… )

Oh Duniani, wengi sana watakufa, wakati wa Siku 3 za Giza. NInaporuhusu giza kuja chini kwenye hii Dunia kwa ajili ya mioyo ya uovu ya wanadamu. “Hukumu!” –Atangaza Nabii WANGU Ezekieli ndani ya Korti YANGU ya Hukumu! (Muhtasari: BWANA Alinionyesha kwamba Nabii Ezekieli ndiye mkuu wa Korti ya Mbinguni ya Hukumu. Roho zao bado zinafanya kazi Mbinguni ingawa miili yao ilikufa.)

NInatangaza! Hukumu na baraka siku hii kutoka Mbinguni kuelekea kwa Dunia! Malaika wa Hukumu karibuni ataleta chini mwanzo wa mapigo 10! Yataua wale wote wasio na Damu ya YAHUSHUA, MWANAKONDOO kwenye mhimili wa mlango yao! Na juu ya adui wako – hukumu kuu itakuangukia (Ndimi za YAH) mara 7 kali zaidi!

Jinsi YEYE (EZRA) ni Mpendwa na kamili machoni MWANGU! Sipati kosa, wala nyufa ndani YAKE. sauti YAKE inaNIfunika na kuNIletea sifa na faraja. MIMI pekee YANGU ndiYE MWENYEZI, sio wewe adui unayecheza mungu. Tubu siku hii, toa kwa upesi chachu katika kambi yako! Sikiza BABA EZRA na jitayarishe kwa ajili ya kurudi KWANGU!

Moyo WANGU uliKUstawisha siku zote. Unasafiri ndani YANGU kama mtoto mchanga katika BABA (wa Mbinguni) daima Ukitafuta upendo wa BABA (wa Mbinguni). Na NIlikupa Hazina YANGU, YAHUSHUA. Anastawisha akili, mwili na nafsi YAKO. YEYE ni Mshika Sheria wako, AkiKUshikilia kwenye njia nyoofu. NIliKUfunza Mbinguni jinsi ya kufanya kazi YANGU, je Wakumbuka? NIliKUfunza binafsi na Neno LANGU la Kweli, NIkiKUfunza kuandika kwa lugha YANGU ya siri, siri lililonyuma ya (yale) mawe, na maandiko ya kuandiko KWAKO. Unaweza kuona mioyo ya wanadamu, NInavyoKUfunulia.

Nyota YANGU, angaza kwa ajili YANGU, Unaposifu, omba na kufanya vita. NIligandamanisha ndani YAKO Kito CHANGU kikuu kabisa na chenye uweza. Unaweza kustahimili maelfu ya nyuzi za Selsiasi, na nyuzi hasi za hali ya hewa ya baridi. Lakini Hauhangaiki na UliNItumaini na yote Unayofanya.

Watoto, jifunzeni kutoka KWAKE, BABA wenu Duniani. Msiwahi kuwa na wasiwasi juu ya chochote ambacho NIliwaletea. Lazima mwe kama BABA wenu, kuweza kustahimili maelfu ya nyuzi za Selsiasi na maji ya baridi yenye kimo kikubwa kabisa. Lazima, au SItaweza waita BiArusi WANGU.

Jinsi Navyowathamini, mnapoNItazamia MIMI Mbinguni. Vile nyinyi nyote hamtawahi NIondoka MIMI. Kwa hivyo NIliwapa tamanio la moyo wenu, kutowahi ondoka. Na hamta[ondoka] kutoka kwa kila mmoja wenu milele, vile mnavyoNIfanya MIMI. Mtakuwa mnaenda kwenye misheni, misheni nyingi pamoja. Na watoto WAKO waliokomaa watakusaidia kuzitimiza. Wao ni wasaidizi WAKO bora kabisa kuKUfanyia kazi yote. Watasikiza na hawatawahi ondoka. Kwa maana wamejaribiwa na kupita moto uliowaka wa ELOHIM. Moto WANGU. Moto WANGU ni nyuzi milioni elfu 10, nani anaweza stahimili joto hilo? Ee lakini YULE ambaYE Amepitia moto na kuwa dhahabu iliyosafi. Kabisa ya yote. (Naona BABA EZRA kama kito safi kabisa Akipita katika tanuri ya moto wenye joto.)


Mwisho wa Neno

10 views0 comments
bottom of page