top of page

Unabii 5 “Yerusalemu, Uasi wa Kukosa Shukrani!”

Umepewa Nabii Hannah kwa Sifa, Heshima & Utukufu wa ELOHIM (MUNGU) Mbinguni


Umeandikwa Januari 20, 2019

Muhtasari


BWANA Anazungumzia kuhusu kundi la watu ambao Alitumia BABA EZRA kutoka Israel, lakini badala ya kuthamini fundisho la BABA EZRA, waliMgeukia na kusema maneno maovu dhidi YAKE. YAHUVEH Anazungmza na watu hao ambao ni waasi dhidi ya Kiongozi Alichagua.


Ujumbe wa Kinabii


BABA Achora msalaba kwenye vipaji vya nyuso zetu, nilisikia “Alama ya Ushindi”)

“NImekasirika! Sio tu kwa matendo yao, lakini kukosa shukrani kwao! NIliwapa kila kitu! NIkatuma NABII WANGU kutoka Israeli (BABA EZRA)! NIngeMtuma pahali pengine. Lakini moyo wao usio na shukrani utaleta kifo chao. NItaangamiza mipango yao. Jiji lao la dhahabu walilojenga. Hawatasitawi.

Wanafikiri wao wote ni wenye nguvu kama tu jeshi la Loki (Kutoka kwa Filamu ya Thor, yeye ni ndugu-nusu mwasi wa Thor). Mwasi kabisa, mwenye kiburi kabisa. SItaruhusu BiArusi wa aina hii!

Ee Yezebeli, ni wapi unaelekeza watu wako? Je, ni pale MIMI YAHUVEH Nawaelekeza? Mguu wako uko katika maji ya tope, usipogeuka, utakufa. Sio kifo cha kimwili bali cha kiroho.

NIna huruma zaidi juu yako. Maana umetumika kama msemaji, lakini unajua bora zaidi kuliko hii. Chagua tu kutosikia Maneno YANGU na Sauti YANGU. Lakini Nitafanya Manabii WANGU kupaaza sauti na wazi kwenye mtandao!

Tubu, mwanamke! Umeenda kwenye eneo hatari! Kama vile kulungu huingia eneo la mwindaji, umelengwa. Na ‘bila jina’ na yule mbwa mwitu mwengine.

Yote kwa sababu ya kutotii. Haikuhitaji kufanyika. Lakini lazima NIruhusu kile NIliahidiwa na YAHUSHUA.

(YAHUSHUA) Atatimiza kazi, NImeisema tu sasa hivi. Utainama, sio EZRA WANGU. Wajiona wewe nani kuambia EZRA kuinama na kukusihi wewe? Nani alikupa mamlaka hayo?

NItakunyenyekeza kama mume juu ya Yerusalemu. Na kuchukua tena kile ambacho ni CHANGU kihaki.

Huyu Nabii anavyosema, hivyo itakavyo kuwa. Natangaza siku hii, ufalme wako utaangamizwa. Umetengeza mungu wako juu ya tovuti. Lakini NItaiondoa kwa muda kidogo hadi EZRA WANGU Atakapokuja, halafu atarejesha kila kitu kama Nehemia wa Kale. Alichukuwa nyundo ya dhahabu katika mkono mmoja na patasi katika huo mkono mwingine.

NInapendezwa wakati NInaposikilizwa. Si wengi wanataka kusikia sauti YANGU tena. Lakini unataka, NInakufundisha. Sasa nenda, na uwaambie Ujumbe huu kutoka kwa BABA yako YAHUVEH.”

Mwisho wa Neno

2 views0 comments
bottom of page