top of page

Unabii 19“MIMI YAHUVEH Nasema, ‘Ikiwa Mnakataa Sheria ZANGU, MnaNIkataa MIMI!’”

Umepewa Nabii D’vorah kwa Sifa, Heshima & Utukufu wa ELOHIM (MUNGU) Mbinguni


Umeandikwa 14 Februari, 2019

Maandiko Husika

Mathayo 5:17-19 “Msidhani kwamba NImekuja kufuta Sheria au Manabii; Sikuja kuondoa bali kutimiza. Kwa maana, amin Nawaambia, mpaka mbingu na dunia zitakapopita, hakuna hata herufi moja ndogo wala nukta itakayopotea kwa namna yoyote kutoka kwenye Sheria, mpaka kila kitu kiwe kimetimia. Kwa hiyo, yeyote atakayevunja mojawapo ya amri ndogo kuliko zote ya amri hizi, naye akawafundisha wengine kufanya hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni, lakini yeyote azitendaye na kuzifundisha hizi amri ataitwa mkuu katika Ufalme wa Mbinguni.

Mathayo 19:16-21 “Mtu mmoja akamjia YAHUSHUA na kuMuuliza, “MWALIMU Mwema, nifanye jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?” YAHUSHUA Akamjibu, “Mbona unaNIuliza habari ya mema? Aliye mwema ni MMOJA tu. Lakini ukitaka kuingia uzimani, zitii amri.” Yule mtu akaMuuliza, “Amri zipi?” YAHUSHUA Akamjibu, “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, waheshimu baba yako na mama yako, na umpende jirani yako kama nafsi yako.” Yule kijana akasema, “Hizi zote nimezishika. Je, bado nimepungukiwa na nini?” YAHUSHUA Akamwambia, “Kama ukitaka kuwa mkamilifu, nenda, ukauze vitu vyote ulivyo navyo, na hizo fedha uwapemaskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, uNIfuate.”

Warumi 10:9 “Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba “YAHUSHUA ni BWANA,” na kuamini moyoni mwako kwamba MUNGU AliMfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.”



Muhtasari

Kukupa wazo ya mbona Unabii huu ulitokea, kuna tamaduni ya Kiyahudi kwamba “kutokuchanganya nyama na maziwa na bidhaa zake”, na ilitokana na Kutoka 23:19. Torah inatuamuru: “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake” (Kutoka 23:19). Torah inapiga marufuku kukula nyama na maziwa kwa pamoja, na hata yapiga marufuku kitendo cha kuvipika pamoja (pia kutoa faida fulani kutokana na mchanganyiko kama huo). Kama kinga, Wahenga walikataza kukula nyama na maziwa na bidhaa zake mlo mmoja, au kuvitayarisha na vyombo vile vile. Kwa hivyo, jikoni ambamo ni kosher lazima liwe na seti mbili tofauti za sufuria, vikaango, sahani na vyombo vya fedha – moja ya nyama/ kuku, mabata n.k. na hiyo nyingine ya vyakula vya maziwa.


Ujumbe wa Kinabii



(Nilikuwa nimekaa kwenye paja la ABBA YAHUVEH Mbinguni na Alikuwa na huzuni. Aliniambia kwamba sina wazo kuhusu uchungu ambao Anateseka. NiliMuliza, “Naweza fanya nini Kukufariji?” Alinionyesha Watoto WAKE wakitumikiana katika maono Mbinguni nilipokuwa nikiketi kwenye paja LAKE, na Akasema, “Mnaweza tumikiana kama Watoto WANGU.”

Halafu nikauliza Paulo – kwa sababu Mtume Paulo aliingia katika hicho chumba – “Paulo, unataka kutufunza nini?” Akasema…)

Ufafanuzi wa Tanakh (Bibilia). Ee, nasikitika! Nasikitika na jinsi wanavyogeuza maneno yangu na kudai nilisema tusishike Sheria za Torah na Sheria za Kosher!

‘Usichanganye nyama na maziwa na bidhaa zake’ ni Sheria ZANGU za Kosher, Asema BWANA YAHUVEH wa Majeshi, MWAMBA wa zama zote, MUNGU wa Shalom. Ni kisingizio kusema kwamba mimi sikufanya vitu hivi wakati nilikuwa mwangalifu wa wote. Usidharau mianzo midogo, mpendwa.

Mimi ni Paulo, na mimi ni yule mwanaume aliyesamehewa. Usiwahi tazama nyuma kwa yaliyopita. Kwenda mbele Binti. Unataka ujue jinsi mimi, Shaul, nilifanya? Sikuwahi kumbuka maisha yangu ya nyuma wala sikuyafunga katika yale mapya.

Unahitaji Maji YANGU Yaliyo Hai, Asema YAHUVEH, kufanya ubongo mpya. Wakati uchovu unakuja juu yako na unahisi mchovu, NIpe kelele ya sifa, hata ikiwa ni akilini – na NItainua shela ya giza ya usingizi inayofunika ubongo. Shika kila wazo tiifu chini ya mamlaka YANGU na NIpe mamlaka ya kufanya hivyo.

Ee, jinsi NInavyokupenda! Jinsi NImekosa wakati wako wa pekee na MIMI YAHUVEH, na MIMI YAHUSHUA! Pata kuTUjua zaidi Binti! Ee, jinsi NInavyokupenda! Wewe ni wa thamani machoni MWANGU na macho yako ni macho YANGU na NItakuhimili na kukufunika na kukuficha chini ya Mabawa YANGU ya Utukufu. Nakupenda tunu WANGU.

Mwisho wa Neno

4 views0 comments

Recent Posts

See All
bottom of page