top of page

Unabii 92 MWAMBA wa WOKOVU na MWAMBA wa UWEPO

Updated: Mar 24


Umepewa Nabii Natan’El kwa Sifa, Heshima & Utukufu wa ELOHIM (MUNGU) Mbinguni

Umepokewa usiku wa Shabbat mnamo 13 Novemba, 2020



Maandiko Husika


1 Petro 2:4-8

4 Mmwendee YEYE [YESHUA], jiwe lililo hai, lililokataliwa

na wanadamu, bali kwa MUNGU ni teule, lenye heshima.

5 Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa muwe nyumba ya Roho,

ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho,

zinazokubaliwa na MUNGU, kwa njia ya YESHUA HAMASHIACH.

6 Kwa kuwa tena imeandikwa katika Maandiko:

“Tazama, Naweka katika Sayuni JIWE KUU LA PEMBENI, teule, lenye heshima,

Na kila amwaminiYE hatatahayarika.”

7 Basi, kwenu ninyi mnaoamini, YEYE ni wa thamani. Bali kwao wasioamini,

“Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa JIWE KUU LA PEMBENI.”

8 Tena, “Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.”

Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini,

nao waliwekwa kusudi wapate hayo.


Zekaria 4:6-7

6 Akajibu akaniambia, akisema, “Hili ndilo neno la

YEHOVAH kwa Zerubabeli, kusema, ‘Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu,

bali ni kwa ROHO YANGU,’ Asema YEHOVAH wa majeshi.

7 ‘Nani wewe, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli

utakuwa nchi tambarare! Naye atalileta lile

JIWE LA KUWEKWA JUU KABISA pamoja na vigelegele vya,

“Neema, neema, ilikalie!”



Ujumbe wa Kinabii


Kunyweni kwa vimo, ee watu WANGU! Msitelekeze matangi maji ya urembo, ya utukufu ambayo NImechonga kwa Mkono WANGU mwenyewe wa Kulia, kwa Mkono WANGU mwenyewe wa Kushoto. Kunyweni kwa vimo na mjifariji katika METATRON. Kunyweni TAV kwa kimo na msitelekeze manufaa YANGU. Noneni katika Neno LANGU lakini msihodhi. Shirikini na watu WANGU, manabii WANGU.


Maana kwa muda mrefu mmenenepa kwenye ufunuo, siri za ufalme, za utaratibu, za kumbukumbu za halakha. Farijini watu WANGU, hivyo Asema MIMI, YEHOVAH. Achilia mzingo.


Njoni mjikinge chini ya MWAMBA – MWAMBA wa WOKOVU WANGU, MWAMBA wa UWEPO WANGU na ruhusini UTUKUFU WANGU kupita juu yenu, kupita mbele yenu. Nawaita KWANGU katika jangwa. Kunapo pahali pema zaidi pa kupumzika? Ambapo mwili umesulubiwa. Njoni nje ya kambi (Waebrania 13:10-13). Njoni KWANGU, ee Israeli. Kamwe SIchoki kuwaita, kuwaashiria mje KWANGU. Kwa maana NImevutiwa na urembo wenu. NIliwavisha. NIliwapamba. Njoni KWANGU, ee Israeli, Bi-Arusi WANGU wa thamani. Njoni KWANGU na msitazamie mwingine, msitazame kulia wala kushoto.


MIMI ndiye kila kitu mnachohitaji. Sujuduni mbele ZANGU. MIMI ni MUNGU wenu, ELOHIM wenu Aliyejaribiwa na Mkweli. Na karibuni NItawatumia Wajumbe WANGU, Wajumbe WANGU wa agano. Mliwatafuta hapo mbeleni – hawa wakombozi (Obadia 1:22). Sikiliza malaika mpiga mbiu akiimba. Wakombozi hawa waja wakiwa wamebeba mawe za Uwepo. Je, mtawasaliti? Je, mtawagusa (dhuru)? Ee Israeli, msithubutu! Msithubutu kugusa WANGU waliotiwa mafuta (1 Nyakati 16:22).


Tazamia kilicho chenu na msitamani [cha mwengine]. Je, haikuwa kwa ajili ya wivu YESHUA Alisalitiwa (Marko 15:6-11)? Je, haikuwa kwa ajili ya ulafi wa mali? Ee Israeli, Naweza endelea. Mfanyakazi si mkuu kuliko bwana wake, wala mwana juu ya babake (Yohana 13:16). Ee Israeli, je, nyinyi si wanaNGU? Je, mko juu ya Neno LANGU? Someni Neno LANGU, Torah YANGU ndio, lakini msifasiri kulingana na kiwango chenu, kwa maana hili ni uhaini, hili ni kukufuru. Neno la MFALME linasimama lenyewe na halihitaji ufasiri wa mwili. Roho, NIpe Roho.


Acheni “ndio” yenu iwe “ndio” na “la” yenu iwe “la”. Zaidi ya hili ni dhambi, ee Israeli (Mathayo 5:37)! Msiguse WANGU waliotiwa mafuta na wala msidhuru manabii WANGU. Nawaonya kabla NIpige. Msianguke katika mtego uliowekwa mbele zenu na adui wenu, adui wa nafsi yenu. yeye ni mjanja. yeye ni mwenye hekima katika kutenda uovu. Ee Israeli, amewapeleka wapi? Je, hamjabebwa bebwa na kila upepo wa mafundisho, kila dhoruba la wimbi la bahari (Waefeso 4:14)?

Wapi amani yenu? Wapi uthabiti wenu? Ni kwa sababu mmetelekeza visima mlivyochimbiwa na mkono WANGU wenyewe, na mkono wa MUUMBA wenu – YULE Awapendae, Awatakasae (Yeremia 2:13). MIMI, YULE UMOJA. NIsikie, ee Israeli, na msikanyage pale ambapo SIjaenda. Fuateni hatua ZANGU. Fuateni utaratibu WANGU. Msitafute michoro yenu ya faida yenu wenyewe. NIsikizeni na mjue MWANAKONDOO. MWANAKONDOO wa MUNGU yuko hapa kuishi. YESHUA HAMASHIAKH BEN YEHOVAH (Yohana 1:29-34).


Fuateni Torah YAKE. Fuateni METATRON WAKE. Nawapa uzima – MIMI, MTUNGAJI. Msitafute mauti, kwa maana SIpatikani huko. Chagueni uzima (Kumbukumbu 30:19). Chagueni baraka. Chagueni YULE MMOJA – MIMI, EKHAD. Chagueni na mwekwe huru mnapoweka mtazamo wenu, jicho lenu juu YANGU (Hesabu 21:8-9, Yohana 3:14-15). Selah.


Maelezo: MWAMBA wa WOKOVU ni YESHUA JIWE la KUU la PEMBENI na MWAMBA wa UWEPO ni METATRON JIWE la KUWEKWA JUU KABISA.


Mwisho wa Neno.


21 views

Recent Posts

See All
bottom of page