top of page

Unabii 25 “Ghadhabu YANGU Iko Dhidi Yenu, Enyi Sayari za Uovu, Asema MIMI, YEHOVAH!”

Updated: Apr 14

Umepewa Nabii Natan’El kwa Sifa, Heshima & Utukufu wa ELOHIM (MUNGU) Mbinguni

Umeandikwa 29 Machi, 2019


Ujumbe wa Kinabii

Ninyi nyote makaidi, chukizo, enye hisia [zaidi] [za huzuni] – sayari za uovu – Nitawameza nyinyi nyote na kuwatema nje upande saba tofauti! Mnafikiri SIwezi weka sayari [nzima], milki nzima katika Kisaga Nyama CHANGU, Shinikizo LANGU la Gadhabu?! Tazama, Nafanya kitu kipya! Tazama Nafanya kitu kipya, Asema, MIMI, YEHOVAH! NItawapasua vipande vipande NInapochonga ardhi yenu, milki yenu na mitetemeko ya ardhi na maonyesho ya Gadhabu YANGU mifano yake ambayo hakuna sayari imeona au kupitia mbeleni. NIna mpango hususan kwa ajili yenu – sio kwa wema bali kwa uovu, sio kwa kufanikisha bali kwa kuteteketeza na uharibifu.


NInawaona! MIMI, YEHOVAH, NInawaona mnapotafuta kuchezea Israel WANGU, na Aliye dhati Machoni MWANGU. Mwathubutu vipi?! Yeye ni WANGU, WANGU, WANGU!

NIsikieni, ee Israeli! MIMI, EKHAD, ELOHIM wenu, Nawaambia, Nawaamrisha kukoma kupeana kile ambacho SIkuwapa kupeana! NItawaadhibu kwa ajili ya hili, NItawavunja, ee Israeli! Nalia, Naomboleza kwa ajili ya kile lazima NIfanye kuwanyenyekeza, kwa kuwa damu nyingi sana itamwagwa kote nchini, kote duniani kupata usikivu wako, kukuleta kwa magoti yako na chini zaidi ili utatubu mbele ya uso WANGU – MIMI, ADONAI HASHEM YEHOVAH. Jinsi NInavyohuzunikia Binti WANGU mpweke, mkaidi … Kutaabika, huzuni, dhiki nyingi sana ingeweza kuepukwa ikiwa tu angetubu, angetubu tu.


Lakini sasa Nazungumza na Biarusi WANGU, Biarusi WANGU wa Milenia mrembo na Bikira mtakaso, wa dahari za zama – daima mwaminifu na mkweli, mrembo wa umbo, mavazi ya kujisitiri, kwa maana anavaa Mavazi ya Uadilifu, ya uadilifu na nasaba ya BABA yake. Endelea Biarusi WANGU, Malkia WANGU. Kutawazwa kwako hakuko mbali, na utatawala na MIMI kando YANGU. MIMI – KICHWA chako, na – wewe mfupa wa mifupa YANGU na mwili wa mwili WANGU, roho wa ROHO WANGU. Ee jinsi NImevyokungojea na kukutamani sana. Biarusi WANGU mtakaso, Bikira wa Utakatifu, Binti wa Haki ya Mfalme.


Inuka, inuka, inuka, Mrembo WANGU, urembo wa zama, furaha ya moyo na nafsi YANGU! Njoo KWANGU, MUUMBA na MFALME wako, MUME wa Shamba la mizabibu, MWEKA Ukweli na Maisha yenyewe. Ungana NAMI, Mrembo WANGU, na ufurahie furaha za BABA YANGU.


NAKUITA, KWA maana Kufika KWANGU hakuko mbali. Je, wasikia sauti YANGU katika nyimbo na tuni za mambo ya asili? Vitu vyote vilivyoumbwa vinagumia, vinalilia kwa sauti kudhihirishwa kwa Wana na Mabinti wa MUNGU. Inuka Mzuri WANGU, mrembo WANGU. Njoo naMI kwa Chumba CHANGU, maana NInakunyoshea Fimbo YANGU ya Kifalme. Je, unapokea huu mwaliko, haya makazi ya amani na ghanima?




Mwisho wa Neno


8 views

Recent Posts

See All
bottom of page