top of page

Unabii 80 “Tahadharini Pigo la 8 la Nzige, Ee India na Marekani!”


Umepewa Nabii TORAH KEEPER kwa Sifa, Heshima & Utukufu wa ELOHIM (MUNGU) Mbinguni

Umeandikwa 9 Machi, 2020


ABBA YEHOVAH Alinena nami na kusema:


“Dhoruba kubwa yaja.”


Nilipomuona katika maono kwenye kiti CHAKE cha enzi, niliona moshi ukipanda kutoka chini ya kiti cha enzi wakati Alikuwa Akinena nami na kusema hili katika hayo maono. Alisema,


“Dhoruba kuu yaja India, ile ambayo haijawahionekana mbeleni.”


Niliuliza ABBA YEHOVAH ni aina ipi ya dhoruba inakuja India? Alinena nami tena na hili neno likatokea:



Ujumbe wa Kinabii


Hakuna mvua, pigo la 8. Nzige wanazungukazunguka angani. NItafunga anga za India. Nzige watakukula ee India! Kwa hivyo msiwe katika utulivu! Kwa maana mapigo yatakuja karibu na makazi yenu kuleta uharibifu kwenye nchi. Nzige watakumeza hai ee Marekani! Kuweni tayari kwa siku zijazo watoto WANGU! Jificheni katika safina ya usalama. NIkiri MIMI na acheni Nielekeze njia zenu. Nimewaficha ndani ya METATRON, ikiwa kweli nyinyi ni WANGU. Mtajificha chini ya kivuli cha mabawa YANGU, Malaika WANGU Mkuu METATRON wa utukufu Anakaa juu ya Marekani na dunia. Ingieni chini ya usalama wa hayo mabawa (Zaburi 91) na msisumbuke na ndwele iliyoko baharini, lakini NItumainie kuwaficha na kuwalinda kutokana na pigo la nzige.


Ee India, ee India, kizuizi kikubwa kitatendeka! Taifa lako halina uti wa mgongo! NItavunja uti wa mgongo wa India! NItamkata kwa msumeno mara mbili kama vile tu mmefanya neno LANGU. Na sasa ee India, Nakuua!


Limeanguka, limeanguka, ee taifa Kuu la Babeli (Ufunuo 18:2)! Poromoka chini kutowahi inuka tena! Behemothi! Vuguvugu! Nakutapika kama sumu, mbali na midomo YANGU! Kwa ajili ya sumu yako na usaliti wako utaonja kifo cha mzaliwa wa kwanza. NItakupiga India kwa siku chache tu na pigo LANGU la 8. Kuweni wenye busara kama nyoka na wasio hatia kama njiwa (Mathayo 10:16) na muingie katika safina ya usalama ya METATRON – watoto WANGU WOTE wa utukufu katika India. Tulieni na mjue kwamba MIMI ni MUNGU (Zaburi 46:10)!


Mungu wa wale vuguvugu Ashteroth! NItabomoa nguzo zake (Kumbukumbu 12:3)! NItaharibu nchi za jangwa la Ashuru – itaenea kote duniani (Isaya 37:18). Msiwe kama Waashuru, ee dunia! Marekani imekuwa kama Siria! Mavimbe na mapigo yake ni ndwele za maambukizi yakitona sumu ya unafiki na dhambi yake. Ee Marekani, NInakuchukia sasa kwa maana kile ambacho ni chako si tena CHANGU! Kwa hivyo Nakutaabisha kama vile katika siku za Moshe na laana za Kumbukumbu 28 na hata zaidi kuja. Kwa maana kiburi kimemeza mataifa! Kwa hivyo gaagaa na ulie ee Marekani! Kwa maana saa yako ya siku ya maangamizi i hapa!


Msiogope enyi watoto WANGU wadogo! MIMI YEHOVAH, Nasema, “Shhh usiogope Nafariji nafsi yenu (Isaya 43:1). Jificheni tu kwa muda kidogo zaidi ghadhabu YANGU inapopita dunia. Kuweni tayari kwa maana dunia ya baharini haijapumzika na haipumziki. Kuweni tu haraka kumaliza hiyo kazi; watoto [WANGU] wachanga, Bi-Arusi, wachaguliwa na wateuliwa WANGU wanahitaji kuonywa! SIsimamishi dhoruba na pigo la 8 hadi ghadhabu YANGU itulizwe. MIMI YEHOVAH NItachukua kisasi juu yako ee Marekani! Ni siku chache tu – katika saa 1 NItakuondoa kutoka kwenye ramani na kukutia alama kama taifa la wakiwa (Ufunuo 18:2).


(Naona maono ya moshi ukipanda juu katika patakatifu kabisa.)


Uchumi wa Marekani utaanguka. (Naona maono ya taa za mafuta huendassss 4-5 zikija chini toka mbinguni) na zimejazwa na mafuta YANGU ya hasira! Kuweni tayari kuonja ghadhabu YANGU ee dunia! Mashahidi WANGU 2 wako hapa tayari! (Ufunuo 11:1-14) Wanawajia kuwapiga kwenye mipaka yenu na kuwapiga mapigo katika mitaa yenu hadi mwishowe muinamishe magoti yenu KWANGU! MIMI ni YEHOVAH na NIna shahidi! NItawapamba kwa vito na johari katika utukufu kabla warudi kwenye sayari Dunia na kupitia wao kwa taifa hili NInafanya kuzaliwa upya! Fundisho la zama mpya, usayansi, momoni, shamani, waajinabi, waangalizi waovu, viumbe wa baharini, walozi wanawake, wachawi wanaume, waabudu shetani, Waashuru, jueni hili na mnaweza hakikishwa, wakati safina YANGU ya usalama inarudi na JINA LAKE ni METATRON, Atawateketeza ee ulimwengu, ee Dunia! Na wakati Anapuliza itaunda mwagiko mwingi wa ghadhabu YANGU kwa Mataifa (Ufunuo 11:4-6)!


NInatuma pigo la 8, NInafungua mihuri (Ufunuo 5)! Kwa maana uangamizaji umekuja ee Marekani! Kwa hivyo tayarisheni vyakula vyenu, tayarisheni maji yenu, kwa watoto WANGU wa kweli wakati unaenda kuwa mgumu.


Watazama Nyota wako hapa. Watawakataa [kwa dharau] na kuwapiga na pigo la 8, mapigo yote, udhaifu, magonjwa hadi mwishowe muinamishe goti lenu KWANGU, MUNGU mkuu NDIMI NILIYE YEHOVAH ELOHIM!


NIombeni MIMI ee Wahindi! (Na kwa Waislamu) Geukeni kutoka kwa Uislamu na mgeuke kutoka kwa allah! Geukieni Yehova, ukweli ee Mashahidi wa Yehova! MIMI YEHOVAH NItawaponda kwa kubadilisha neno LANGU, kulipanga upya neno LANGU!


Kuweni kama simba-jike NIkazieni fokasi! NIkazieni fokasi kwa maana NIna mambo mengi Naenda kuwaonyesha leo. (Naona maono ya ndovu akiwa na maji katika mkonga wake.)


Ee Marekani, kuweni tayari! Kwa maana tangi lenu la maji ya uzima kutoka mbinguni linaanza kufunga. Maporomoko theluji yataanguka kule Alaska na mbadiliko wa ncha za dunia ufanyika. Mataifa mengi yatavuna maangamizi, yatavuna kile yamepanda. Kama NIlivyosema mbeleni watoto WANGU, soko la hisa hivi karibuni kabisa litaanguka Marekani. Kuweni tayari, jitayarisheni.

Mwisho wa Neno.

©2019 by Torah Keeper.

bottom of page