top of page

Unabii 39 YESHUA Asema, Mbingu Yakaribisha Watoto wa MUNGU Waaminifu!

Updated: Apr 14

Umepewa Nabii Hannah kwa Sifa, Heshima & Utukufu wa ELOHIM (MUNGU) Mbinguni

Umeandikwa 24 Mei, 2019


Ujumbe wa Kinabii


Nilisikia YESHUA Akiambia watu duniani:


“Mpendwa WANGU, waona! Nilikushindia dunia, ili uweze kukombolewa kutokana na majaribio ya kila aina. (YESHUA Atabasamu). Mpendwa WANGU (Niliona Akiinama chini na kuinua wale waliokuwa wameanguka chini). Hauwezi kuwa adui wako mwenyewe [na] mbaya zaidi, hauwezi jiumiza. Moyo wako si wako tena, ni WANGU. Kwa hivyo ikiwa moyo wako ni WANGU, utafikiria kuNIhusu na moyo na akili yako yote. MIMI ni MWOKOZI wako, YESHUA HAMASHIAKH. Nilikufa msalabani, na nikafufuka kwenye huo msalaba. Upendo WANGU – kubwa kuliko dhahabu – Upendo WANGU – haubadiliki kamwe. Kwa hivyo Mpendwa WANGU, sikiliza nabii WANGU. Nakupenda. Nawapenda enyi watoto WANGU wote mliopo China, Taiwan, Singapore, Japani na Korea!


Sikilizeni Maneno ya watoto WANGU kutoka Huduma ya Torah Keeper! Nitainuliwa na watu wote wataNIabudu!

MIMI ni MWOKOZI ambaYE hatawahi badilika, YESHUA HAMASHIAKH. Na huyu nu nabii WANGU anayetumikia kila mtu. Yeye ni mpendwa WANGU. Mtendeeni vyema kama vile mnaNItendea. Kuweni wema kwa manabii WANGU. Msiache manabii WANGU walie. Kwa sababu mnahitaji maji wanayowapa, na wao pia wanahitaji muwape kikombe cha maji.


Msisahau, ee dunia! Mpinga-kristo atatokea! Yuko mahali karibu sana, anaonekana Marekani, Israeli, Waziri Wakuu, Rome, Vatican n.k. Hamjui ni nani mnaenda kukabiliana naye au ni nini mnaenda kukabiliana nacho. Dunia inatazamana na vita. MIMI ni MUNGU AsiYEbadilika. Sisemi kuwa nyinyi si WANGU – mradi msiNIache – basi nyinyi daima ni watoto WANGU! Ufalme WANGU wa Mbinguni unakaribisha wale wanaotii amri ZANGU!


Angalia, Sikuja duniani kwa ajili YANGU, bali kuokoa wanadamu. Lakini wakati Nitakapo rudi tena, mtaona MIMI ni simba mkali. Nitararua maadui WANGU. Ee Xi Jin Ping, hadhari! Ningojee pamoja na bibi na binti yako. Nimekasirika sana nawe. Ee uliua watoto WANGU! Watoto WANGU duniani, mko na damu YANGU. Kwa sababu mna DNA na nasaba YANGU. Dhabihu yenu haijapotea bure! Saulo WANGU atakuwa Paulo. Yote kwa sababu ya wafia dini Watakatifu. Walilaza maisha yao chini. (Niliona maono ya mhubiri mweusi akiuawa kishahidi Afrika). MwanaNGU, George WANGU, Nakupenda! Uko kwenye barabara ya kuenda Mbinguni. Hii haiko mbali sana!


Nawapenda enyi watoto WANGU. Hii [huduma] ni ya manabii wa Enzi Mpya. Tazameni, ee dunia. Dunia itapitia maafa, tsunami, mitetemeko mikubwa ya ardhi...


Niliwacheleweshea haya kwa muda mrefu sana. Lakini mliNItendea vipi, ee watu? Mnaendelea kutenda dhambi, mnaendelea kuNIudhi. Nilituma manabii WANGU wanaosikia sauti ZANGU kuwaonya kwenye Huduma ya Torah Keeper.

New York endelea kungojea. Ee ngojea, Nitangojea ile siku mtaNItupa mbali. Hiyo ni siku ya karibu kuja. Ee na Nilisema mbeleni, RUAKH HAKODESH WANGU Atakuacha kabisa! Ngojea hiyo siku, New York. Wakati huo, hakuna atakayeokolewa na hakuna atakayetaka kuokolewa. Kila kitu kinafanyika New York ni njozi na uongo! Nabii WANGU hakuisema makosa. [Neno] lolote! Manabii WANGU, maneno Ninayoweka mdomoni mwenu kama vile maneno ya hukumu au upendo, lazima myaseme yote!


Kwa sababu upako WANGU, upako WANGU uko hapa.

Utakuwa Biarusi WANGU, Bibi WANGU Mpya. Watoto WANGU wachanga, watoto WANGU, Nawapenda. Ndio [YESHUA Anatabasamu].


Hizi ni siku zijazo za karibu. Kwa kweli haiko mbali. Je, mwaNIngojea? Ndio, mnaNIngojea na mtaendelea kuNIngojea. Shalom, watoto WANGU. Fuateni hii Huduma na mtaona karibuni...


Mwisho wa Neno


9 views

Recent Posts

See All
bottom of page